Pages

Ads 468x60px

.

About

.

ADVERTISE HERE!

LOOKING FOR INCOMES? MARKETING OR PRODUCT PENETRATION? INCREASE YOUR MARKET BY CONNECTING YOU TO US, US TO MILLIONS OF SUBSCRIBERS ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE

ADVERTISE HERE

LOOKING FOR INCOMES? MARKETING OR PRODUCT PENETRATION? INCREASE YOUR MARKET BY CONNECTING YOU TO US, US TO MILLIONS OF SUBSCRIBERS ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE

ADVERTISE HERE!

LOOKING FOR INCOMES? MARKETING OR PRODUCT PENETRATION? INCREASE YOUR MARKET BY CONNECTING YOU TO US, US TO MILLIONS OF SUBSCRIBERS ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE

ADVERTISE HERE!

LOOKING FOR INCOMES? MARKETING OR PRODUCT PENETRATION? INCREASE YOUR MARKET BY CONNECTING YOU TO US, US TO MILLIONS OF SUBSCRIBERS ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE

ADVERTISE HERE

LOOKING FOR INCOMES? MARKETING OR PRODUCT PENETRATION? INCREASE YOUR MARKET BY CONNECTING YOU TO US, US TO MILLIONS OF SUBSCRIBERS ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE

Featured Posts

.

Wednesday, August 8, 2012

WB yaipa Ilala Sh41Bilioni kuboresha miundombinu

BENKI ya Dunia (WB) imetoa mkopo wa Sh41 bilioni kwa ujenzi  wa miundombinu Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam.

Fedha hizo ni sehemu ya Sh150 bilioni ambazo ziliombwa na halmashauri nne za Dar es Salaam kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la madiwani,  Meya wa Ilala, Jerry Silaa alisema Serikali iliomba mkopo WB kutekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha miundombinu ya Da es Salaam.

Slaa alisema miundombinu hiyo ni barabara, mifereji ya maji, uzoaji taka, urasimishaji makazi, uboreshaji mapato ya halmashauri, ujenzi wa miundombinu kwenye makazi yasiyopangwa na utawala bora.

“Uboreshaji miundombinu ya barabara na mifereji ya maji ya mvua, zimetengewa Sh21 bilioni, ukusanyaji na usafirishaji taka ngumu umetengewa Sh5.3 bilioni, uboreshaji miundombinu kwenye makazi yasiyopangwa Sh 8.4 bilioni,” alisema Slaa na kuongeza:

“Urasimishaji na kutenga maeneo ya huduma kwenye makazi yasiyo rasmi imetengwa Sh1.6 bilioni.” 
Pia, alisema mradi huo ni wa awamu ya kwanza ambayo itahusisha kata za Kiwalani, Gongolamboto  na Ukonga na kwamba, wakimaliza wataingia awamu ya pili.

“Uboreshaji huo utakuwa Kata ya Kiwalani mitaa ya Minazi mirefu, Yombo, Kiwalani na Kigilagila; Kata ya Gongolamboto itahusu mitaa ya Gongolamboto, Ulongoni, Guluka Kwalala na Mongolandege na Kata ya  Ukonga mitaa ya Makazi, Mazizini na Mwembe madafu,” alisema.

Naye Diwani wa Kata ya Kivule, Nyasika Getema alisema kwenye kata yake ametengewa Sh6.29 milioni  kwa ujenzi wa barabara ya Mombasa-Moshi bar.


Saturday, July 28, 2012

RAMBO AMZIKA MWANAE 


STAA, Sylvester Stallone Rambo, amemzika mtoto wake wa kwanza, Sage Stallone, ambaye alifariki baada ya kumeza madawa mengi. 

Sage ambaye amewahi kuigiza na baba wake katika filamu ya Rocky V, alifariki dunia mapema mwezi huu ikiwa ni siku chache kabla ya kufunga ndoa. 
Chanzo cha kifo chake hakijathibitishwa na daktari, isipokuwa maiti yake ilikutwa pembeni ya chupa tupu za vidonge zipatazo hamsini. Sage amefariki akiwa na umri wa miaka 36. 
Kama alivyo baba yake, naye alikuwa mwigizaji, mwongozaji na mtayarishaji wa filamu.


CHAMELEONE ATINGA UBALOZINI



Mwanamuziki wa Nchini Uganda,Jose Chameleone (ambaye hivi karibuni alikuwepo hapa nchini kwa shoo yake moja) leo amefanya maandamano mpaka Ubalozi wa Tanzania nchini Uganda akiambatana na wapenzi wa muziki wake,kwa lengo la kutaka kurudishiwa Passport yake inayodaiwa kuwa inashikiliwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Publishers,Erick Shigongo.


Hapa akizungumza na askari wa Ubalozini hapo.Inasemekana kuwa Shigongo aliamua kuchukua uamuzi huo wa kuchukua passport ya Jose Chameleone kwa kuwa Meneja wake alimtapeli kiasi cha dola 3500 kipindi cha nyuma hivyo ameamua kuzuia pasport yake mpaka atakapomleta Meneja wake huyo. Mwanamuziki Jose Chameleone akipiga gitaa lake na kuimba huku wapenzi wa muziki wake wakiwa wamemzunguka kushinikiza Ubalozi wa Tanzania nchini Uganda kufanya taratibu za kuwezesha kupatikana kwa hati yake ya kusafiria (passport) inayoshikiriwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Publishers,Erick Shigongo.






Tuesday, July 3, 2012


NHC KUUZA NYUMBA KWA BEI NAFUU


SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) lina mpango wa kujenga nyumba 15,000 hadi ifikapo mwaka 2015 na kuziuza kwa bei nafuu kwa wananchi wenye kipato cha chini.

Mkurungenzi Mkuu wa shirika hilo Nehemiah Mchechu alisema Jijini Dar es Salaam jana kuwa nyumba hizo zitaanza kuuzwa kati ya Sh25milioni hadi Sh40 milioni  kwa lengo la kumsaidia mwananchi wa kipato cha chini.

Baada ya kusaini mkopo wa Sh165 bilioni kutoka kwenye Taasisi tisa za kifedha,Mchechu alisema fedha hizi zitawasaidia katika mradi wa ujenzi wa nyumba na ununuzi wa ardhi ya akiba katika mikoa mbalimbali nchini.

“Nyumba tulizojenga zaidi ya 1,500 kwa mwaka huu  zimewalenga wananchi wa kipato cha chini yule ambaye atashindwa kununua nyumba ya Sh70,000 ataweza kununua nyumba za bei nafuu ambazo zitauzwa Sh25 hadi 40 milioni”alisema na kuongeza;

“Mradi huu wa ujenzi umeanza kutekelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Kigoma ,Arusha na Dodoma huku miradi mingine ipo njiani kutekelezwa” alisema Mchechu

Pia alisema kati ya fedha hizo zilizotolewa  Sh23 bilioni zitapelekwa  kwenye ujenzi wa nyumba za bei nafuu ambazo nyumba hizo zitawalenga wananchi wa kipato cha chini.

Kwa upande wake  Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof Anna Tibaijuka alisema wananchi wametakiwa kununua nyumba badala ya kununua viwanja ili kuepuka gharama zisizokuwa na  msingi.

Waziri huyo alisema wananchi wataweza kukopa nyumba hizo ambazo mikopo yake italipwa kwa riba ya chini ili waweze kunufaika na mradi huo.

“Wananchi wanunue nyumba badala ya  kununua viwanja, hii  itamrahisishia kupunguza gharama ya kununua kiwanja na kujenga ambayo kiwango chake ni kikubwa”alisema Profesa Tibaijuka.
 Profesa Tibaijuka alisema kati ya nyumba hizo zinazojengwa asilimia 25 zitabaki kwa ajili ya watu ambao watahitaji kupanga.


Monday, July 2, 2012

UVUMI KUHUSU JUSTINE BEIBER


Kumenea kwa uvumi mbalimbali kuhusu mwimbaji huyu na amefikiria kuimba wimbo utakao shika mawazo ya jamii
Justine Beiber hivi karibuni anakabiliwa na shtaka kutoka kwa msichana kuwa yeye ni baba wa mtoto wake, Ilikuwa aibu kwa na vigumu kukubali kwa nyota huyu ambaye anakuwa. Sasa ameamua kutafuta njia mbadala itakayo weza jibu maswali yake kwa kuimba wimbo utakao ongelea matukio yalio muhusu Justine Beiber na atatoa ufafanuzi juu ya yote kwa njia ya mistari ya wimbo wake!

Justin Bieber amepokea umaarufu mkubwa kutoka kwa mashabiki ndani ya kipindi kifupi sana, sasa ana kwa ana atajitahidi kujisafisha kwenye skendo mbalimbali zilizo muhusu yeye.


MADEREVA WALIOKAMATWA ZAMBIA


CHAMA cha Madereva wa Malori (Chamamata) kimeiomba Serikali kufanya utaratibu wa kuwarejesha madereva waliofungwa nchini Zambia ili waje kutumikia vifungo vyao hapa nchini.Hivi karibuni, chama hicho kilitishia kufanya mgomo kushinikiza kuachiwa huru kwa madereva hao lakini kimesitisha baada ya kubaini kuwa walitoa tamko hilo kinyume cha sheria.


Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa chama hicho, Clement Masanja alisema madereva 12 walifungwa mwaka jana nchini Zambia baada ya kupatikana na hatia ya kufanya uchakachuaji wa mafuta ya mawese.
Alisema mafuta hayo yalikuwa yanasafirishwa na kampuni ya Dando na kwamba magari 14 yalikamatwa na madereva wawili walifanikiwa kutoroka.  
“Tunaomba serikali itusaidie kufanya utaratibu kati yetu na serikali ya Zambia ili wenzetu waje watumike vifungo vyao hapa nchini,” alisema Masanja.


Alisema pia matajiri wengi wamekuwa wakiwaonea madereva hali iliyosababisha waishi maisha magumu na kuingia kwenye vishawishi kutokana na kipato kidogo.
“Hebu fikiri dereva anasafirisha mzigo kwenda Congo anakaa siku 60 analipwa Sh200,000 tu je ataweza kukidhi mahitaji yake?” alihoji Masanja.
Kuhusu kusitisha mgomo wao, Mwenyekiti huyo alisema walibaini kuwa mtu waliyekuwa wanamshinikiza awaachie huru wanachama wao (kampuni ya Dando) hana uwezo huo kwasababu madereva hao tayari wamo mikononi mwa sheria.


Naye mmoja wa wajumbe wa chama hicho, Hussein Msangi alisema hivi karibuni alienda nchini Zambia na kukutana na baadhi ya wafungwa hao na kwamba wengi wao walikutwa wana hali mbaya kiafya.
“Kuna mwenzetu mmoja anaitwa Edward Mwakibinga tulikuta anaharisha damu na kama ikitokea hata mmoja akafa kuna hatari ya watu kugoma,” alisema Msangi.
Alisema madereva hao wamefungwa kwa shoti ndogo kati ya lita 100 na 160 wakati madereva wengine walikutwa na lita 70 za maji ambazo alidai kuwa ni kitu cha kawaida kwenye mafuta.


 
 
Animated Social Gadget - Blogger And Wordpress Tips